bc

JAKAMOYO NA HADITHI NYINGINE

book_age18+
0
FOLLOW
1K
READ
family
drama
mystery
like
intro-logo
Blurb

DIBAJI

Katika kitabu chake cha hadithi fupi, “Maskini Milionea”, Hamisi Babusa anaelezea bayana

kuwa, Afrika ni bara la fasihi simulizi. Hivyo wengi wetu tumeishi na kulelewa katika mazingira

ya kumegewa tanzu za fasihi simulizi k,v vitendawili,. Ngano, visasili, hekaya na hurafa.

Hadithi fupi ni hadithi zilizobuniwa na kuwasilishwa kwa lugha nadharia ya masimulizi.

Maneno haya yanaenda sawia na anavyoelezea mhakiki maarufu wa asili ya kiafrika, Abiola

Irele, kuwa hadithi fupi ni zao la utamaduni wa fasihi simulizi.

Hadithi fupi husimuliwa katika mtindo wa ploti ya moja kwa moja, tofauti na riwaya (novela),

ambayo husimuliwa kwa mitindo changamano.

Hadithi fupi husimulia kuhusu tukio moja tu linalotukia katika kipindi kifupi katika maisha ya

mhusika.

Hata hivyo, kuhusika kwa wahusika wachache ni sifa moja nyingine bainifu ya hadithi fupi. Hii

hutokana na kutokuwepo kwa muda wa kutosha wa kukuza wahusika wengi kama ilivyo katika

novela. Tujuavyo, wanadamu wana mazoea ya kusimuliana hadithi kila wanapotangamana na

jamii. Hivyo, hadithi zinazotufikia katika mfumo wa kitabu cha hadithi fupi kama mkusanyiko

huu wa “Siri ya moyo na Hadithi nyingine”, ni hazina kubwa inayokidhi utashi wetu wa kutamba

na kutambiwa hadithi.

Mkusanyiko huu wa matukio ni simulizi mbalimbali kwa njia ya fasihi andishi, inayoburudisha

na kuadilisha msomaji yule yeyote, na hivyo kuwa kama bibi na babu wa kutusimulia hadithi

kwa njia ya kitabu.

Ni jukumu kuu kwa wale wanaonzi kiswahili na maandishi ya Kiafrika kwa jumla kwamba, ili

waweze kupata uhondo uliomo ndani mwa fasihi andishi, ni sharti wawe na uzoefu wa

kuchambua na kubukua vitabu aina aina ili kujiweka katika muktadha wa misamiati, misemo,

vitendawili, misimu na ngano mara kwa mara na kumwezesha msomaji kukuza lugha kwa

mapana.

Wewe kama msomaji, unapopata fursa ya kupitia nakala hii ya hadithi fupi ya “Siri ya moyo na

hadithi nyingine”mwandishi Ally, ni ombi la mwandishi kwamba upate kuimarika, kumakinika

na kupata muda wa kutosha ili kwa kina uchambue kila sehemu pasi kusahau kumegea jirani

yako yale yote mazuri utakayokumbana nayo na kuzoazoa katika usomaji.

Shukrani za dhati kwako msomaji. Ni tumaini langu kuwa utaweza kukusanya mengi ya uadilifu,

uchochezi, ukosoaji na hata ya kulaani visa vingi vinavyotendeka miongoni mwa wanajamii

visivyo vya manufaa na elimu kwa kizazi kipya.

Endelea kukikuza Kiswahili. Endelea kuienzi lugha na pamoja twaboresha Kiswahili.

Wako mhariri,

Allan M. Ingutia.

AllyIM

March 28, 2020.

chap-preview
Free preview
ZAWADI HERI NJEMA
Ilitokea siku ambayo tajiri mmoja alikisia kufanya mapenzi na mjakazi wake anayesaidia kusafisha afisini mwake. Mjakazi huyo kwa jina la Zora, aliwahi kazini ambako ni Ofisi kwa muajiri wake na kisha kuendeleza kazi za usafi kabla tajiri kufika. Tajiri alipofika dakika chache tu, kabla ya Zora kukamilisha usafi, alimpa mkono kwa salamu. “Hujambo dada?” Alimsalimu Bw. Kababa. “Mara haba Bwana Mkubwa.” Alijibu kwa ustaarabu Zora. Lakini jambo lililomstaajabisha Mjakazi ni kuwa, alipompa mkono Bw Kababa kwa heshima ya salamu, Bwana huyo hakuweza kuuachilia mkonowe Zora kwa wepesi. Salamu kwa mkono, ulibadili maudhui ya kazi na kutawala manthari ya kuchumbiana. Wafanyavyo wapenzi, Bw Kababa aliubana mkono wake Zora kisha akamkazia jicho lililoeleza kwa bayana hisia za kwake. Ama kweli usilolijua jambo ni sawa na usiku wa giza. Dakika chache, walionekana wote wameambatana kuelekea garini. Haikosi muda huo ofisini kulitokea maelewano ya kimapenzi baina yao. Siku hiyo, wengi wa wafanyakazi chini ya uongozi wa Bwana Kababa, walisalia kutikisa vichwa vyao huku wamebana midomo lisitokee la kutamka kutokana na kisa hicho. Siku iliyofuatia, minong’ono ilienea kote mjini Kazamwendo, jinsi wawili hao walivyojistarehesha mnadani Pumzika Resort. Haikosi ilihesabika siku ya kwanza kwake Zora kukionja kinywaji chenye makali mpaka kujisahau. Kilichofuatia ni wote wawili kuzinduka usingizini na kujikuta chumbani mwa Bwana Kababa hasa kitandani. Asubuhi hiyo hamna aliyekuwa na jawabu ni jinsi gani wamejikuta pale na nini hasa kilichotukia walipokuwa mle chumbani. Aisee! Haikosi Bwana Kababa alipata fursa ya kusoma katiba kwa ustaarabu usiku huo. Wote wawili walionekana kujawa na maswali sufufu Kupitia nyuso zao zilizoeleza masikitiko makali. Waama, majuto ni mjukuu, huja baadaye. Ikawa Sasa imepungua miezi miwili mwakani elfu Kenda mia tisini na nne. Zora alianza kuhisi dalili za uja uzito. Ingawa mwanzoni hakuelewa manake aliishia kusikia kutoka kwa Wengine kuhusu uja uzito, na hapo yalimfika yeye. Alijaribu kuvumilia hali hiyo lakini ikamzidi. Alikata kauli ya kuenda zahanatini kupata jawabu mwafaka. Alistaajabishwa sana mara daktari alipomueleza, yeye ni mama mtarajiwa, na angejifungua miezi sita mbeleni. Kwa kweli, mtoto wa watu angefanyaje ilhali yalikuwa yameshamwagika, na kamwe hayangeweza kuzoleka. Alikubali hali hiyo, na Kupiga guu mosi guu pili, hadi kazini afisini kwa Bw. Kababa. “Welcome mammy…” Kwa madaha alimkaribisha mjakazi afisini kwake huku furaha imemtawala usoni mwake. Kwa upande mwingine Zora alivalia tabasamu la bandia. “Shukran Mkuu.” Alijibu Zora. “Hivi ni siku mbili Sasa haven’t seen you at work, nini kikubwa labda? Aliuliza bwana Kababa. “ Ni kweli usemavyo mkuu, sijaweza kufika kazini kama ilivyo ada yangu. Ila samahani, naomba nisiyanene mengi. Labda tu nikutaarifu kuwa, mimi ni mja mzito. “What!!!.... Eti unasemaje… Labda sijakupata hebu rudia!...” Aligutuka bwana Kababa. “Ndiyo… Mimi ni mja mzito, na wewe ndiye mwenye majukumu kwa taarifa yako.” Alisema haya huku ananing’inia machozi mbooni mwake, lakini machozi hayo, hayangeweza kuzuilia tetesi zake Bwana Kababa. Alishinikiza kwamba yeye hana lolote wala hahusiki na uja uzito wa mjakazi wake. Alifungua droo na kitita Cha pesa, kisha akampa Zora na kuamrisha aavye mimba ile. Wasemavyo, aliyetapakaa kinyesi ovyo, husahau ila kwake yeye aliyekanyaga, kamwe huishia kukumbuka. Kwa heshima na taanzia za kwake, Zora alipokea pesa zile, na kisha akaondoka zake. Ingawa mwingi wa majonzi lakini lisilobudi. Alipoteza kazi na kusalia omba omba ili asitiri uja uzito mpaka kujifungua. Alhamdulilahi! Mola hamuachi mja wake. Zora alibarikiwa na mtoto wa kike. Alimpa jina Zawadi. Ikawa siku moja, Zawadi na mamake Zora, wanaandaa chajio. Zawadi alibadili hali ya kwake ghafla. Haikosi mawazo yake yalitalii mbali na kwao. Kisha alimuuliza mamake, “Nataka kufahamu aliko baba…wenzangu wameishia kuniita Mwanaharamu. Baba yuko wapi?” Kweli swali hili lilimzungusha Bi. Zora darmadaru kisha likamueka sawa. Alishindwa ni wapi ataanzia kueleza aliko baba mtu. Kilioonekana ni machozi yaliyomtoka na kutiririka kuwili shavuni mwake. Zawadi naye nani, alikazia na swali lake. Bi. Zora alieleza yalitokea mwanzoni mpaka akamzaa Zawazi. Alimuonyesha baadhi ya picha za Bwana Kababa kabla ya tukio. Alimpa matumaini ya kumpata babake ila shingo upande.

editor-pick
Dreame-Editor's pick

bc

Unscentable

read
1.7M
bc

He's an Alpha: She doesn't Care

read
649.5K
bc

Claimed by the Biker Giant

read
1.3M
bc

Holiday Hockey Tale: The Icebreaker's Impasse

read
886.8K
bc

A Warrior's Second Chance

read
312.0K
bc

Not just, the Beta

read
318.7K
bc

The Broken Wolf

read
1.1M

Scan code to download app

download_iosApp Store
google icon
Google Play
Facebook